.post-body{ -webkit-touch-callout: none; -khtml-user-select: none; -moz-user-select: -moz-none; -ms-user-select: none; user-select: none; }

0
Kampuni ya chakula Heinz imeomba msamaha baada ya alama ya siri katika mkebe mmoja wa Tomato Ketch Up kuwaelekeza wateja katika mtandao wa ngono.
Kampuni hiyo hiyo imesema kuwa alama hiyo ya siri ilipitwa na wakati na kwamba illikuwa inatumia kila njia kuhakikisha kuwa kitu kama hicho hakifanyiki tena.
Swala hilo liligunduliwa na na Daniel Korell,mteja wake nchini Ujerumani ambaye aliripoti kwa kampuni hiyo.
Swala hilo lilibaini hatari inayoweza kusababishwa na alama hizo za siri kulingana na mtaalam mmoja wa usalama.
Alama hiyo ambayo inaweza kupatikana kwa kutumia simu aina ya Smartphone ili kuweza kuingia mtandaoni ilitakiwa kuwaelekeza wateja katika eneo ambalo watumiaji wanaweza kubuni lebo ya chupa ya Heinz Tomato Ketchup Hot kama mpango wa ukuzaji wa bidhaa hiyo unaofanywa na kampuni hiyo.
Aliripoti kisa hicho akisema kuwa huenda bidhaa hiyo haiwafai watoto wadogo.

Post a Comment

 
Top