.post-body{ -webkit-touch-callout: none; -khtml-user-select: none; -moz-user-select: -moz-none; -ms-user-select: none; user-select: none; }

0
Mawasiano ni jambo muhimu sana kwa maendeleo ya ulimwengu, njia za mawasiliano ni pamoja na barabara, simu, mazungumzo, ujumbe mfupi, barua, barua pepe, bahari, reli, tovuti, na vituo vya mawasiliano vingine.
Njia hizo zote za mawasiliano zina faida na ubaya wake.
Hebu na tuangalia VITUO VYA MAWASILIANO, ambavyo wengine wanasema ndio njia bora zaidi ya kuwasiliana. Kuna mamia ya vituo vya mawasiliano, na kituo maarufu zaidi-facebook-kinakadiriwa kuwa na washiriki wapatao milioni 800! “Ikiwa facebook ingekuwa nchi, kwa mujibu wa time magazine, inasema ingekuwa ni nchi ya tatu kwa ukubwa duniani, baada ya china na india.” Vituo vya mawasiliano ni nini, na kwanini vimekuwa maarufu sana?
Kituo cha mawasiliano ni tovuti inayowezesha washiriki kusambaza habari zaokati ya marafiki ambao wamewachagua. Pia kituo cha mawasiliano hutumika kuwaonesha wenginee picha zako aidha za mahafali, au safari yako ulivyokwenda likizo kijijini, au matukio mengine.
Kuandika barua kunachukua muda mrefu kufika lakini pia itakugharimu ikiwa unataka kutoa nakala nyingi ya picha, kupiga simu kutakugharimu kwa kuwa utalazimika kumpigia mtu mmoja mmojana huenda wengine wasiwe hewani au wasipokee simu zenyewe na wakawa hawana wakati wa kuzungumza nawe wakati wewe una muda. Siku hizi si watu wengi wanaojibu  barua pepe, na hata wakifanya hivyo huenda ikachuku majuma mengi hadi mtu kukujibu. Lakini unapotumia vituo vya mawasiliano, unapachika tu maelezo yako, kuhusu mambo unayoyafanya na marafiki zako nao watapachika habari na picha zao, na kila mmoja ataweza kuona kwa haraka taaifa na habari zote pia picha. Na nyinyi nyote mtaweza kupata habari kwa haraka tena mara moja mnapoingia katika aidha tovuti au kituo hicho cha mawasiliano na ni rahisi sana hakuna gharama kubwa.
Hilo halimaanishi kuwa mazungumzo kupitia vituo vya mawasiliano huwa ni upuuzi mtupu. Kwa mfano, msiba unapotokea, kama vile sakata la mabomu gongo la mboto, mimi nilikuwa katika semina ya walimu iliyoandaliwa na british council iliyofanyika huko bwawani morogoro, na mafuriko yaliyotokea juzi mimi nilikuwa jijini Istanbul nchini uturuki, lakini nilizipata kwa haraka taarifa kupitia vituo vya mawasiliano, na nikaweza kujiona hali halisi kupitia picha zilipachikwa humo. Watu wengi hutumia vituo vya mawasiliano ili kufahamu hali za wapendwa wao au kutafuta marafiki wapya nap engine kujua ni kiasin gani anapendwa.
Ni dhahiri kuwa, kuna faida za kutumia vituo vya mawasiliano, lakini pia tujiulize, je kuna hatari zozote? Ikiwa zipo, ni hatari gani hizo na unawezaje kuziepuka?
“Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na kosa, lakini anayezuia na kuchunga ulimi wake ametenda jambo la busara zaidi”
VITUO VYA MAWASILIANO VINAATHIRIJE UNDANI WAKO?
Usipokuwa mwangalifu, habari zako za kibinafsi, picha, ujumbe mfupi unaopachika kwenye ukurasa wako, na maelezo unayoandika kwenye ukurasa wa wengine, yanaweza kufunua mambo mengi sana yakuhusuyo ambayo hukuyatarajia. Kwa mfano, yanaweza kufunua habari kuhusu mahali unapoishi, wakati ambapo upo nyumbani, ama ikiwa umetoka, mahali unaposoma au kufanyia kazi, habari kuhusu mahali unapoishi pamoja na ujumbe kama vile “Kesho tunaenda likizo” unatosha kumwambia adui mahali na wakati wa kukushambulia.
Kufichua habari nyingine kama vile anuani ya barua pepe, tarehe ya kuzaliwa, au namba yako ya simu kunaweza kufanya udhulumiwe, uonewe,  au kumfanya mtu aibe utambulisho wako. Ingawa watu wengi hutoa habari hizo kiurahisi katika kurasa zao za vituo vya mawasiliano.
Watu husahau kwamba mara tu wanapopachikakitu kwenye intaneti, kinaweza kupatikana na kila mtu. Hata mtu anapofunga ukurasa wake utumike na watu maalum tuau marafiki pekee, hawezi kudhibiti jinsi marafiki hao watakavyotumia habari hizo. Kwa kweli chochote ambacho mtu anapachika kwenye kituo cha mawasiliano afahamu kuwa kinapaswa kuonwa na kuwa ni habari ya umma au habari ambayo umma unaweza kuipata kwa urahisi zaidi.
VITUO VYA MAWASILIANO VINAATHIRIJE WAKATI NA FIKIRA ZAKO?Image result for hd computer photo
 “Mhakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi, maana wakati ni mali”
UNACHOPASWA KUJUA.
Kutumia vituo vya mawasiliano kunaweza kukuibia wakati mwingi sana na kukukengeusha kutokana na utendaji mwingine muhimu zaidi. Ukiwa na marafiki wengi ndivyo utakavyotumia wakati mwingi zaidi katika kituo cha mawasiliano na ni rahisi zaidi kuwa mraibu. Nilifanya utafiti mfupi kuhusiana na namna watu walivyonaswa na utumiaji wa muda mrefu katika vituo vya mawasiliano na kusahau kuwa wana majukumu mengine, wasikilize hawa:
“Ni vigumu kuacha kutumia uso wa kitabu-facebook, hata wakati ambapo hutaki kuendelea kukitumia kituo hicho au umechoka, na ukiacha ni pale unapokuwa umepitiwa na usingizi” Julieth-Osterbay
“Kuna vitu vingi sana unavyoweza kufanya humo-michezo, mitihani, kurasa kwa ajili ya watu wanaopenda muziki Fulani, kazi za ulinganiaji wa kidini, bila kutaja kurasa za marafiki wako, lakini utaacha yote hayo ya muhimu na kupoteza muda kwa rafiki hata kukiwa hakuna cha kukijadili” Mwinchumu-Tabata
“Ni uraibu unaokunasa kabisa pasi na mwenyewe kufahamu, hutambui kuwa umenaswa hadi mama yako anaporudi nyumbani na kukuuliza kwanini hujaosha vyombo” Hawa-DUCE
“Nilijikuta nikitamani kufika nyumbani upesi kutoka shuleni na hata saa zingine kuona mwalimu wa kipindi cha mwisho ni kero darasani ili nikaone ikiwa kuna yeyote ambaye ameandika maelezo yake kwenye ukurasa wangu au anasubiri kuchati na mimi. Kisha nilihitaji kuwajibu wote hao na kuangalia picha zote mpya walizopachika. Ilikuwa ni rahisi sana kwangu kuudhika nilipokuwa nikitumia intaneti, na nilichukia sana mtu aliponikatiza kwa aidha kunituma au kutaka jambo hata kuniongelesha. Watu Fulani ninaowafahamu hutumia kituo hichi kila wakati-hata wanapokuwa wamealikwa, katika vikao, maofisini, madarasani na pia usiku sana, muda wote utawakuta wapo hewani na ukiwauliza wanakujibu papo kwa hapo!”- Fransis-Mbande secondary
Hakika utakubaliana name kuwa mara nyingi umekuwa ukifikiria kujisomea, lakini mara ulipokumbuka kuwa kuna watu watakuwa wamekutafuta fb, ukaachana na habari ya kujisomea na matokeo yake ukajikita katika kuchati na kupandishwa picha hadi usingizi ukakupitia
Hakika wakati ni kitu ambacho hupaswi kukipoteza,
 KWA HIYO NI JAMBO GANI UNALOWEZA KULIFANYA KUKABILIANA NA HILI?

JAMBO UNALOWEZA KUFANYA. 
Image result for hd computer photoWakati ni kitu ambacho hupaswi kupoteza. Kwahiyo, kwanini usipange jinsi utakavyoutumia, kama unavyoweza kukaa na kupanga namna utakavyotumia pesa zako baada ya kuzipata? Kwanza, andika kiasi cha wakati unachohisi kwamba kinafaa kutumiwa kwenye kituo cha mawasiliano. Kisha jichunguze kwa mwezi mzima na uone ikiwa ulitumia wakati vizuri kama ulivyopangilia. Fanya mabadiliko yanayohitajika.
Ikiwa wewe ni mzazi na vijana wako wanatumia wakati na muda mwingi kwenye vituo vya mawasiliano, jaribu kuchunguza ikiwa kuna mambo yoyote yanayochochea tatizo hilo. Kwa mfano, katika kitabu chake CYBER-SAFE KIDS, CYBER-SAVY TEENA, Bw Nancy E Willard anasema kwamba kutumia kituo cha mawasiliano kupita kiasi kunaweza kuhusianishwa na wasiwasi, mfadhaiko, na kutojiheshimu. “Vijana wengi huwa na wasiwasi kuhusu ikiwa wanapendwa na wengine au la,” anaandika. “Ikiwa vijana wanapima kama wanapendwa kwa kutegemea wanawasiliana na marafiki wao kwa kiwango na kadiri gani kupitia vifaa vya kielektroniki, hilo linaweza kuchochea uraibu.”
Usiache vituo vya mawasiliano-au utendaji wowote wa intaneti-uathiri uhusiano unaopaswa kuwa ukikuza ndani ya nyumba yako mwenyewe. Jambo moja la kushangaza kuhusiana na intaneti ni kuwa ingawa inafanya kuwasiliana kuwe rahisi zaidi wakati ambapo watu wa familia wako mbali, matumizi ya intaneti yanaweza kuwafanya watu au marafiki watengane wakiwa pamoja kwakuwa kila mmoja atashughulishwa na marafiki zake wengine wa vituo vya mawasiliano.”
Nafikiri vituo vya mawasiliano ni njia nzuri sana ya kuwasiliana na watu. Lakini, kama tu kitu kingine chochote, unapaswa kujua wakati wa kuacha kukitumia
.
AFADHALI KUBAKI NI SIFA NJEMA KULIKO KUW NA MALI NYINGI
Mambo mengi unayoyapachika katika kituo cha mawasiliano hukufanya uwe na sifa ambazo si rahisi kuzibadili, Ni kana kwamba watu wengi hawaoni hatari iliyopo. Inaonekana kwamba watu wanapoanza kutumia kituo cha mawasiliano hupoteza uwezo wao wa kufikiri, wanasema mambo mengi ambayo kwa kawaida hawangeweza kusema, wanapachika picha zenye mavazi ambayo kikawaida si muonekano wao. Pengine hawatambui kuwa kupachika kitu kimoja tu kisichofaa kunaweza kuharibu sifa yako daima.

Post a Comment

 
Top